Shughuli za utalii za siku za lavender zahimiza maendeleo ya uchumi katika Mkoa wa Xinjiang, China (5)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 16, 2025
Shughuli za utalii za siku za lavender zahimiza maendeleo ya uchumi katika Mkoa wa Xinjiang, China
Picha hii iliyopigwa Juni 14, 2025 ikionyesha shamba la mimea ya lavender katika Wilaya ya Huocheng ya Mkoa unaojiendesha wa Kabila la Wauygur wa Xinjiang, kaskazini-magharibi mwa China. (Xinhua/Ding Lei)

Maua ya mimea ya lavender yamechanua vizuri kwenye mashamba makubwa mwezi Juni katika Wilaya ya Huocheng ya Mkoa unaojiendesha wa Kabila la Wauygur wa Xinjiang, China, ambapo mandhari ya mashamba hayo yanaonekana kama bahari kubwa ya rangi ya zambarau inayopendeza.

Shughuli za utalii za siku za lavender zinahusisha sanaa za maonesho, mashindano ya michezo, na maonyesho ya mali ya urithi huko. Shughuli hizo zimeanza rasmi jana Jumapili ili kwenda sanjari na mandhari hayo ya kuvutia sana ya mazingira ya asili, kuonesha shughuli zinazostawi za mimea ya lavender ya mkoa huo wakati huohuo, na kuhimiza maendeleo ya shughuli za utalii na uchumi za huko.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha